08/12/2023
Ukitazama msimamo wa kundi D lenye timu za Al Ahly, CR Belouizdad, Yanga na Madeama na ukafanya tathmini kwa kutumia hesabu za kimpira, hutopingana nami kuwa Yanga wana nafasi kubwa ya kusonga mbele hatua ya robo fainali.
Kivipi???!!!
Mechi zinazofuata ambazo ni za mzunguko wa 3. Yanga watakuwa ugenini dhidi ya Medeama, wakati huo Al Ahly watakuwa nyumbani dhidi ya CR Belouizdad.
Kutokana na matokeo ya michezo miwili iliyopita, ni wazi kuwa iwe isiwe lazima Yanga wahakikishe wanapata point 3 ugenini mbele ya Medeama. Na wakishindwa kabisa basi angalau wapate point 1.
K**a watatoa suluhu watakuwa na point 2, wakiendelea kushika mkia kwenye kundi lao. Wakati huo Belouizdad wakiwa ugenini dhidi ya National Al Ahl na wakapoteza, basi msimamo wa kundi D utaendelea kuongozwa na;-
1. Al Ahly (7)
2. Medeama (4)
3. Belouizdad (3)
4. Yanga (2).
Kwenye mzunguko wa 4, Yanga watawakaribisha Medeama kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa. Na Belouizdad watakuwa nyumbani dhidi ya Al Ahly. Kwenye mchezo huu naziona point 3 za wazi kwa Yanga, huku Belouizdad wakigawana point na Al Ahly.
Hapo msimamo utakuwa;-
1. Al Ahly (8)
2. Yanga (5)
3. Belouizdad (4)
4. Medeama (4)
Mzunguko wa 5 utawakutanisha Yanga vs Belouizdad kwenye dimba la Benjamini Mkapa, wakati Al Ahly watakuwa ugenini dhidi ya Medeama.
Hapa kwa Mkapa, Yanga hawatotakiwa kupoteza tena mchezo. Watatakiwa kupambana na wahakikishe wanawafunga Belouizdad huku Al Ahly nao wakimchapa Medeama nyumbani kwake.
Hapo msimamo wa kundi D utaendelea kuongozwa na;-
1. Al Ahly (11)
2. Yanga (8)
3. Belouizdad (4)
4. Medeama (4)
Mzunguko wa 6 ambao ndio utakuwa wa mechi za mwisho. Yanga dhidi ya Al Ahly ugenini, Belouizdad dhidi ya Medeama nyumbani.
Hizi zitakuwa mechi za kukamilisha ratiba tu, kwani hata ikitokea Yanga wakapoteza dhidi ya Al Ahly, na Belausdad wakashinda dhidi ya Medeama bado msimo wa kundi D utabaki vile vile.
1. Al Ahly (14) ✅️
2. Yanga (8) ✅️
3. Belouizdad (7) ❌
4. Medeama (4) ❌
Kumbuka hii ni IMAGINATION tu kulingana na hesabu za kimpira. Mwisho wa siku, dakika 90 za mchezo ndio zitakazoamua nani atasonga mbele na nani atabaki?!
NB: Kwenye soka lolote linaweza kutokea.
Na
Kocha wa Boli
Dec 03, 2023