TAECO LTD

TAECO LTD TAECO is an entrepreneurial company found in Tanzania with the aim of providing formal and informal

Printing books, magazines, newspapers, t-shirts, banners, stickers, posters, flyers, caps etc. we educate people about business and entrepreneurship, business consultants, creating and arranging different forums and conferences about entrepreneurship with the aim of helping the primary entrepreneurs

04/01/2019

Amini nakuambia kuwa na plan million ambazo hazijatekelezwa ni kujichosha tu. Mafanikio huja kwa kuwa na wazo murua, kuliweka wazo kwenye mpango kazi, kulitafiti hilo wazo kisha kulifanyia KAZI. Mwaka mpya tuanze na kufanya kazi naamin plan tunazo ni za kufanyiwa kaz tu

Je mwaka unabadilika au mindset inabadilika?Kweli kabisa unasheherekea siku ya kuzaliwa huku hakuna lolote la maana umef...
31/12/2018

Je mwaka unabadilika au mindset inabadilika?
Kweli kabisa unasheherekea siku ya kuzaliwa huku hakuna lolote la maana umefanya? Vivyo hivyo unaposheherekea kuukaribisha mwaka huu mpya basi hakikisha malengo ya mwaka jana umeyatimiliza kwa angalau kuvuka 50% na pia uwe umebaini makosa uliyoyafanya mwaka uliopita ambayo hutoyarudia mwaka huu tena. Vinginevyo huna faida wala umuhimu wa kusheherekea mwaka mpya iwapo mindset yako haijabadilika. Soma zaidi hapa
https://lnkd.in/dXiZdXK
uweze kufahamu mambo matano ya kuzingatia kwa mwaka huu wa 2019. Kheri ya mwaka mpya

book printing and publishing, magazines,newspaper, seminars, events organizers, training and mentoring

01/11/2018

SIO KILA NJIA INABIDI UPITE
Watu hudhani kwamba kila opportunity inayokuja kwako inabidi uitumie kitu ambacho wengi hufeli... Kwanza lazima uainishe malengo yako na njia ambazo unataka kuzitumia kufikia lengo lako. Kwa mfano unakuta mtu anataka kua mwandishi mzuri wa vitabu ila imetokea opportunity ya kuvua samaki anajiingiza, my friend unaelekea kufeli vibaya. Malengo yako sio ya kwanza kuwepo katika dunia hii, Kuna maelfu ya watu walishawahi kuwa na idea k**a yako, tafuta mentors na tumia muda mwingi ku-search watu waliowahi kupublish mambo k**a yako utapata knowledge kubwa sana na utajua pa kuanzia. Mfano mimi mpaka kua mwandishi ambaye nimeshaandika vitabu zaidi ya 48 sikukurupuka ila nilifatilia kila hatua hadi kwa kina Shigongongo kuniwezesha kutambua kipawa changu halisi
So acha kurukia kila njia inayokuja kwako ukiamini itakufikisha unapopataka

30/06/2018

Jaribu kufatilia watu wachache ambao wamefanikiwa kabisa, utagundua walifeli zaidi ya mara elfu katika kuyafikia malengo yao. Leo umefeli mara kadhaa tu unasusa na kukacha ndoto yako kabisa, ndugu hakuna mafanikio ya usiku mmoja. Ili mmea uote lazima ufe na kuoza ndipo ufufuke na kumea, sasa kwa kukacha kila ufelipo bila shaka ndio maana upo hapo ulipo, jitafakari upya - Mtenga Gerald

29/06/2018

Simamia kitu kimoja ambacho unaamini kabisa kinaweza kukuvusha katika bahari hii yenye mawimbi lukuki. Kutapatapa na mambo mengi hakujawahi kumvusha yeyote salama, ukiwa na lengo moja kuu, ukaliamini kwa moyo wote, ukalifunga shingoni k**a tai kisha ukatafuta mbinu mbadala za kulifikia lengo hilo basi hongera upo katika njia sahihi ya kukufikisha ng'ambo salama - Mtenga Gerald

28/06/2018

Ukizungukwa na watu ambao daima ukitoa wazo lako either wanakuambia "hilo mbona haliwezekani" au pia "kwa hali ya sasa ya uchumi itashindikana" na mengineyo basi kaa nao mbali. Kushindwa kwako kunaanzia na kua na negative minded people so jaribu kujiassociate na positive minded people ambao wataona opportunity katika kila wazo lako - Mtenga Gerald

27/06/2018

Kusoma sana vitabu vya biashara, kusikiliza na kuangalia sana video za kuhamasisha pamoja na kusoma blogs mbalimbali za uhamasishaji hakukufanyi ufanikiwe k**a "huchukui hatua" yaani ACTION...fanya maamuzi acha kupoteza muda- Mtenga Gerald

17/06/2018

Marafiki ni chachu ya kukufanya ufanikiwe zaidi au ufilisike zaidi, aina ya marafiki ulio nao ndio inakufanya uwe hivyo ulivyo leo. Jitathmini umesimama upande gani kisha fanya maamuzi sahihi - Mtenga Gerald

29/05/2018

NGUVU YA CPU
Unajua kua ubongo wako ni k**a computer? Yaaan una ram, rom, hard disc na processor...

Computer kile utakachoicommand ndicho kinachofanyika yaaan ukitaka computer yako iwe maalum kwaajili ya video games then all the apps zitakua hivyo, ukitaka iwe kwaajili ya movie then itajaa movies, ukitaka iwe kwaajili ya u-DJ then itajaa kila aina ya nyimbo zote duniani. Yaaan kwa ufupi unachotaka ndicho kinachokua, ndio maana unasikia kuna core i3, core i5, core i7 na zingine means chaguo ni lako... The same applies to your mobile phone. Ila amini kuna watu hawajui matumizi sahihi ya hivi vitu hujikuta anakua na core i7 kwaajili ya kuingia Facebook na social media zingine 🤷🏽‍♂🤷🏽‍♂ hajui jaman usimlaumu

Sasa basi ubongo wako upo hivyo hivyo na kile unachotaka kiwepo kichwani kinakua katika hali ya kawaida maishani mwako. Hivi unategemea ubongo wako uwe umeujaza mambo ya akina Diamond na Ali Kiba sijui Mobetto mara Wema Sepetu utegemee kabisa utakua na uwezo wa kuchangia mada katika seminar ya katiba??? Thubutuuuuu

Jibu la swali la kwanini Wa Africa ni masikini ni simple tunajaza bongo zetu na unwanted materials k**a mipira, udaku, ngono, siasa chafu n.k then tunakosa muda wa kuweka mambo ya uchumi na maendeleo katika bongo zetu

Simple task angalia WhatsApp yako aina ya magroup uliyopo, nenda Facebook angalia aina ya groups na pages ulizolike, nenda Instagram angalia aina ya watu uliowafollow na unaowasearch mara kwa mara then nenda google yako bonyeza pale juu kulia nenda kwenye history angalia aina ya vitu unavyosearch mara kwa mara utapata jibu kwanini bado upo hapo

My friend you are who you are because of what you feed your brain, anza kubadili aina ya vitu hivyo na futa k**a unavyodelete file kwenye computer utaanza kuona kumbe ubongo wako una space kubwa tu ya kuingiza vitu vya msingi

Cha mwisho ni hiki movie moja ukiiweka kwenye computer yako inachukua nafasi ya kuanzia MB 600 na kuendelea ila kitabu kimoja kukiweka huko hakizidi hata MB 10, yaaan movie moja ni sawa na Vitabu 60, jiulize kwenye computer/simu umejaza nini cha msingi cha kushibisha ubongo wako vizuri?...Maamuzi ni yako, chagua sahihi ili usije kujuta baadae.
Siku njema wapendwa

Mr Mtenga
TAECO LTD

26/05/2018

MARAFIKI NA MAFANIKIO
Hivi umewahi kujiuliza ni kwanini mtu anapofanikiwa kwa hatua fulani basi hubadili marafiki na kuachana na wale wa zamani yaaan sio kuwaacha kabisa yaaan kutohang nao tena, na hapa ndio kauli za tangu amepata kazi anaringa mara sasa hivi marafiki zake wa kishua tu sisi ametutupa unajua sababu???

Sababu kuu ni hii, hakuna tajiri hata mmoja duniani amewahi kua na rafiki masikini a big impossible, jaribu kufuatilia histoaria za kina bill gates utabaini rafiki yake mkubwa ni buffet, mengi, barkhresa, mo dewji na wengine utakuta rafiki zao wakubwa ni watu wa kipato fulani, hata Mark wa Facebook sasa hivi rafiki zake ni billionaires wenzake sio wale masikini aliokua nao utotoni

Issue ni hivi ili uzidi kufanikiwa unahitaji booster yaaan mtu atakayekusukuma usonge mbele ila trust me marafiki wale wale uliowazoea watakufanya mtumie hicho ulichovuna na sio namna ya kuongezeka zaidi na zaidi

Ndio maana kwenye siasa tunaambiwa hakuna rafiki wala adui wa kudumu. Acha kukumbatia marafiki zako eti kisa mlikua wote kijiweni wakati huna kitu so now huwezi kuwatupa, brother and sister hutapiga hatua kwa kushikilia mentality hiyo.

Hujawahi kujiuliza kwanini wale wanaojilambalamba na kujipendekeza kuwa karibu na watu waliofanikiwa basi hatimaye nao huwa na mafanikio? The principal is easy "ukikaa na ua Rose lazima unukie" au pia "ukitembea na mwizi nawe ni mwizi" simple logic

Chagua marafiki wapya ambao unajua watakufikisha unapopataka instead of kukumbatia viazi mviringo ambavyo havina faida kwako

Sabato njema wapendwa na siku njema

Mr Mtenga
TAECO LTD

14/02/2018

Je una sifa hizi kumi? Zinaitwa top ten "K's" na mtaalamu Naamala Samson amezifafanua zaidi ila kwa ufupi ni k**a zifuatavyo kwa mtiririko toka 10 mpaka 1

10. Kujitambua
9. Kujituma
8. Kujiendeleza
7. Kuwa tofauti
6. Kuonekana.
5. Kujenga mtandao na watu makini.
4. Kuwa na nidhamu ya fedha.
3. Kushinda hofu.
2. Kutokata tamaa.
1. Kumuweka mungu kwanza.
K**a una sifa hizo zote na hujafanikiwa katika malengo yako basi kuna tatizo mahali, k**a huna sifa hizo au unazo baadhi basi fanya mpango wa kuhakikisha una sifa zote hizo

Address

Dar Es Salaam
10511DARESSALAAM,

Opening Hours

Monday 06:00 - 17:00
Tuesday 06:00 - 17:00
Wednesday 06:00 - 17:00
Thursday 06:00 - 17:00
Friday 06:00 - 17:00
Sunday 06:00 - 17:00

Telephone

0765112177

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAECO LTD posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TAECO LTD:

Share