officiallenath

officiallenath Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from officiallenath, Clothing (Brand), Dar es Salaam.

Kila kitu kitakua sawa ila haiwezi kua sawa k**a zamani Matukio yaliyotokea ni mageni kabisa machoni kwa raia wa Nchi hi...
04/11/2025

Kila kitu kitakua sawa ila haiwezi kua sawa k**a zamani

Matukio yaliyotokea ni mageni kabisa machoni kwa raia wa Nchi hii, Hata mirindimo iliyokua ikisikika wengi wetu tulizoea kuiona kwenye Filamu za Kikorea na Kimarekani ila awamu hii ilifika karibu kabisa

Baada ya Tukio nafsi zetu zimesononeka na Mioyo yetu imejawa na Makovu mengi, Tuliobaki tunaishi hatuwezi kua k**a zamani

Ni siku chache tu lakini tumewakumbuka sana ndugu zetu ambao hawakua na hatia, Tupo tunaishi lakini hatuwezi kuaminiana k**a zamani

Wale tuliamini ni Walinzi kwetu ila sasa tutawaogopa sababu tunajua wanachoweza kufanya muda wowote bila sababu zozote

Moyo umekua mzito kuzungumzia lolote, Kuna Matukio tumeyaona mbele ya macho yetu na Picha zimeganda kichwani 💔😭

Mola wetu, Hili ni kubwa na zito sana kwetu Waja wako Tunaomba utusaidie 🙏

Katika historia ya mwanadamu na hata katika maandiko matakatifu, yapo tofauti kubwa kati ya viongozi wa dini na watumish...
07/07/2025

Katika historia ya mwanadamu na hata katika maandiko matakatifu, yapo tofauti kubwa kati ya viongozi wa dini na watumishi wa kweli wa Mungu.

Tatizo kubwa linalojitokeza katika jamii zetu ni kwamba watu wengi huchanganya hawa wawili kana kwamba ni kitu kimoja. Hii ni hatari, maana si kila anayevaa vazi la kidini au kusimama madhabahuni ni mjumbe wa Mungu.

1. Viongozi wa Dini ni wa mfumo – Watumishi wa Mungu ni wa kweli ya kiroho

Viongozi wa dini mara nyingi wamejikita kwenye kulinda taasisi zao, mamlaka yao, na maslahi yao. Wanaweza hata kutumika k**a vinyago vya nguvu za kisiasa au kiuchumi. Katika Biblia, Yesu aliwakemea vikali Mafarisayo, Masadukayo na walimu wa sheria kwa unafiki na kupindisha sheria kwa manufaa yao binafsi:

"Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnafunga Ufalme wa Mbinguni mbele ya watu; ninyi wenyewe hamwingii, wala hamkubali wale wanaotaka kuingia waingie." – Mathayo 23:13

2. Watumishi wa Mungu wamesimama na Haki, hata ikiumiza

Watumishi wa Mungu, k**a manabii wa zamani – Eliya, Isaya, Yeremia, na Yohana Mbatizaji – waliikemea jamii kwa uovu wake bila kuogopa. Hawakubembeleza mamlaka wala kukubali kununuliwa. Walikuwa tayari hata kufungwa, kuteswa au kuuawa kwa ajili ya kusimamia ukweli wa Mungu. Watumishi wa namna hii ni nadra sana leo.

3. Viongozi wa Dini hutafuta makundi – Watumishi wa Mungu hutafuta nafsi za watu

Viongozi wa dini hujenga maelfu ya wafuasi lakini mioyo ya watu hubaki tupu. Wanahubiri kwa faida, wakigeuza watu kuwa chanzo cha kipato. Lakini watumishi wa Mungu hujenga watu, si majengo wala majina. Huduma yao huzaa toba, haki, na ukombozi wa kweli.

4. Hadithi za Mafarisayo na Masadukayo ni onyo la historia

Yesu Kristo hakuwahi kuwa karibu na viongozi wa dini wa wakati wake. Aliwakemea kwa unafiki wao, kwa kutumia dini k**a silaha ya kuwatesa wengine. Hili ni onyo kubwa kwa vizazi vya sasa – kwamba dini isipotenganishwa na mamlaka ya kiroho, inaweza kuwa chombo cha uonevu na utumwa mpya wa kiakili na kiroho.

Ila   😁😁😊
07/07/2025

Ila 😁😁😊

07/07/2025
12/07/2023

Yoyooo 🌹

   Geita!!!! Nakuja Na Mama Teacher  Rais Wetu Madame PRESDENT  Jumamosi Hiii Uwanjani Pale !!!! Kalangalala 🏟️ IMEDHAMI...
13/10/2022

Geita!!!! Nakuja Na Mama Teacher Rais Wetu Madame PRESDENT Jumamosi Hiii Uwanjani Pale !!!! Kalangalala 🏟️ IMEDHAMINIWA NA OFFICE YA MKUU WA MKOA Hakuna Kiingilio Nishalipwa 💰💰💰 KOPO JUU YA KOPO 😮‍💨😮‍💨💨💨 MAMA ANAMAZUNGUMZO NA NYINYI WANA GEITA BAHATI ILIYOJE !!!!! 🐘

Ahsante sana  na
10/10/2022

Ahsante sana na

Kila Siku Haiwezi Kuwa Nzuri. Lakini kuna Kitu Kizuri Katika Kila Siku✍🏻✍🏻 😁
02/10/2022

Kila Siku Haiwezi Kuwa Nzuri. Lakini kuna Kitu Kizuri Katika Kila Siku✍🏻✍🏻
😁

Chochote cha Bule Maishani kinakuja na Dharau, Jifunze kujipambania 📝
01/10/2022

Chochote cha Bule Maishani kinakuja na Dharau, Jifunze kujipambania

📝

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when officiallenath posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to officiallenath:

Share