ELIMU KWA UMMA

ELIMU KWA UMMA Ukurasa huu unahusu kuelimishana mambo ya mcngi yakiwemo ya dini,siasa,michezo na menginginyo yenye tija ktk jamii.Hairuhusiwi matusi,kejeli na lugha chafu

30/10/2024

Hii ni kwa faida ya umma na aliyeuliza hili in box
Mtume Muhammad (saw) alimwoa Khadija bint Khuwaylid (ra) wakati Khadija akiwa ameolewa mara mbili kabla ya ndoa yao. Mume wake wa kwanza aliitwa Abu Halah bin Zurarah, na mume wa pili aliitwa Ateeq bin Aidh. Hata hivyo, kabla ya kumuoa Mtume Muhammad (saw), Khadija alikuwa tayari mjane, baada ya waume wake hao wawili kufariki.

Wakiwa katika ndoa yao, Mtume Muhammad (saw) na Khadija walijaliwa watoto sita. Watoto wao walikuwa:

1. Qasim – Alifariki akiwa bado mtoto.

2. Zainab – Aliolewa na Abul-As bin Rabi'.

3. Ruqayyah – Aliolewa na Uthman bin Affan (ra).

4. Umm Kulthum – Aliolewa pia na Uthman bin Affan (ra) baada ya kifo cha Ruqayyah.

5. Fatimah – Aliolewa na Ali bin Abi Talib (ra).

6. Abdullah (alikuwa na jina la utani, Tayyib au Tahir) – Alifariki pia akiwa mtoto.

Ndoa ya Mtume na Khadija ilikuwa ya kipekee kwa sababu aliishi naye kwa uaminifu na upendo kwa miaka 25, na hakuoa mwanamke mwingine hadi baada ya kifo cha Khadija.

16/10/2024

Umauti huja ghafula tusilisahau hili

MWANA SIMBA NISIKILIZE.SHABIKI WA SIMBA nisikilize tu kidogo, mpira wa miguu ni burudani lakini kwa upande mwingine ni b...
02/07/2024

MWANA SIMBA NISIKILIZE.

SHABIKI WA SIMBA nisikilize tu kidogo, mpira wa miguu ni burudani lakini kwa upande mwingine ni biashara, anayeipenda klabu ni SHABIKI na anayefanya kazi ya mpira ni MCHEZAJI, mmoja anaburudika na mmoja kati ya hao wawili yupo kibaruani, hata wewe ambaye ni Shabiki una ajira yako pengine sehemu huwa unahama kufuata maslahi mazuri, ndio k**a ilivyo kwenye soka.

CHAMA tayari ameondoka klabuni, ni sehemu ya football ila SIMBA imesalia na itaendelea kuwepo, hata k**a asingeondoka basi kuna siku angestaafu na maisha yangeendelea, ni sahihi kuumia ila ni sahihi zaidi kutopanic na kutupiana lawama yoyote kwa Viongozi au Mchezaji kwakuwa hii ni biashara kuna kukubaliana na kutokubaliana.

SHABIKI wewe ipende hii logo iliyopo kwenye Kila jezi kushoto, fahamu ni wewe pekee hutohama ila wengine woote wanakuja na kuondoka haswa Wafanyakazi wakiwemo Wachezaji, Messi Lionel ameondoka Barcelona, pale Liverpool walimtengeneza Michael Owen ila akasepa zake, Chelsea walimpika Hazard akasepa zake, Man United walimtengeneza Beckham ila akaondoka, timu yangu Arsenal ndio usiseme Nasri ,Fabrigus nawengine na wote walisepa ni kawaida sana kwenye dunia ya mpira.

SIMBA aliwahi kuondoka Juma Kaseja kwenye ubora wake, Emmanuel Okwi kwenye ubora na wengine wengi tu ila klabu iliendelea na wachezaji wengine akiwemo CHAMA ambaye alijenga Ufalme wake, leo umetamatika hivyo klabu itapaswa kuanza maisha mpya na zama mpya, tukubaliane kwa pamoja kuwa nothing is there forever.

Sisi k**a klabu tuna mengi ya kufanya haswa wakati huu focus yetu ni kupaza sauti kuwahimiza wasajili Wachezaji wa maana, tushauri, tukae chini k**a klabu ili tufike sehemu kubwa na nzuri, huu sio wakati wa kunyoosheana vidole wala kupishana bali kuanza mwanzo mpya ambao sote tunautaka, anayehisi hajapenda ahame tu klabu, wala sio suala ila football ni kawaida sana hivi vitu.

Tukae nyuma ya timu, tusupport Wachezaji wote ambao watasajiliwa na tukubali kuwa TRIPLE C ameshaondoka, ila timu haiwezi kufa, maisha yataendelea na tumtakie heri kwenye changamoto mpya.

NGUVU MOJA.

✍️✍️✍️✍️✍️

"GORDON LIU" MBABE WA MOVIE ZA KUNG FU ALIYEKIMBIWA NA FAMILIA BAADA YA KUUGUA MNOKwa wafuatiliaji wa movie nadhan mnamk...
16/05/2024

"GORDON LIU" MBABE WA MOVIE ZA KUNG FU ALIYEKIMBIWA NA FAMILIA BAADA YA KUUGUA MNO

Kwa wafuatiliaji wa movie nadhan mnamkumbuka vema huyu mwamba basi taarifa ni kwamba jamaa mwaka 2011 akiwa na miaka 60 alipata ajali akifanya maonesho ambapo alipigiza kichwa vibaya na kupelekea kuparalaizi na kushindwa kuongea baada ya kuugua mno bila matumaini ya kupona familia yake ilimtelekeza na kugawana mali. Mkewe aliomba talaka akakubaliana na mwanae wa kiume wa pekee na mabinti zake mali zote za jamaa zikauzwa wakagawana mama na watoto na kumkimbia. Gordon Liu ni mzaliwa wa mwaka 1951 huko Hong Kong ni moja kati ya waigizaji wakongwe mno walioshiriki movie nyingi kali za kung fu ikiwemo 36 chambers of shaolin

Kwa sasa Gordon analelewa katika kituo cha kulelea wazee huku akipewa msaada na marafiki zake ambao ni waigizaji maarufu duniani pia. Ana miaka 72 sasa.

Fikiria unapata ajali kazini unaparalaiz halafu familia uliyokua unaipigania inakukimbia inakuacha unakufa mwenyewe kitandan hujitambui

Inasikitisha Sana aisee 😭😭😭

NB:Wakati unatafuta Mali kwa ajili ya warithi wako kumbuka na maandalizi ya kaburi lako


KUNA CHA KUJIFUNZA HAPA😥Jackie Chan alimkaana mwanae kisa alijihusisha na mapenzi ya jinsia moja Jackie Chan alitangaza ...
31/03/2024

KUNA CHA KUJIFUNZA HAPA

😥Jackie Chan alimkaana mwanae kisa alijihusisha na mapenzi ya jinsia moja

Jackie Chan alitangaza kabisa hadharani kua si baba yake tena mzazi wa Etta Ng Chok Lam, tukio hilo lilitokea mwaka 2017.
Na sababu kuu za kutangaza hivo nikutokana na binti yake huyo ni mpenzi wa mapenzi ya jinsia moja na yametokea hayo kipindi ambacho binti yake aliamua kufunga ndoa rasmi na mpenzi wake ambae na yeye pia ni mwanamke k**a yeye . Alichofanya Jackie_Chan alimtimua na kumuondoa kwenye orodha ya watakaorithi Mali zake na kusema kuwa si mtoto wake kuanzia kipindi hicho .
Ikumbukwe kuwa Jackie_Chan anatajwa kuwa na utajiri wa zaidi ya dola za kimarekani milioni 400 .
Kumbuka pia Jackie Chan amemwondoa mtoto wake wa kiume kwenye urithi wa mali zake kutokana na mtoto huyo kutopea kwenye matumizi ya madawa ya kulevya na amegoma kupata matibabu ili aachane na madawa hayo😥😥

Natamani wazazi wote wawe na misimamo hii ya Jackie Chan naamini Dunia ingalinyooka.

From
ELIMU KWA UMMA

{ یَـٰۤأَیُّهَا ٱلَّذِینَ ءَامَنُوا۟ كُتِبَ عَلَیۡكُمُ ٱلصِّیَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِینَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُم...
28/03/2024

{ یَـٰۤأَیُّهَا ٱلَّذِینَ ءَامَنُوا۟ كُتِبَ عَلَیۡكُمُ ٱلصِّیَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِینَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ }
[Surah Al-Baqarah: 183]

Ndugu zangu nimeitafakari sana hii Aya na nimepata mambo matatu ambayo yametajwa ktk Aya hii ukweli wake anaujua Allah kwa hakika.
یَـٰۤأَیُّهَا ٱلَّذِینَ ءَامَنُوا۟. Enyi ambao mmeamini
Hapa imetajwa IIMANI👆
Nani mwenye hakika huyu ameamini zaidi ya Allah
كُتِبَ عَلَیۡكُمُ ٱلصِّیَامُ Mmefaradhishiwa juu yenu
kufunga
👆Hapa imetajwa funga hakuna ajuaye aliyefunga isipokuwa Allah pekee
كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِینَمِن مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ K**a walivyo faradhishiwa waliokuwa kabla yenu
لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ Ili muwe wachamungu
Hapa Allah ametaja TAQWA (Uchamungu)👆
Hakuna mwenye elimi ya kumjua mchamungu isipokuwa Allah.
Amma kwa hakika Allah ni mjuzi wa Kila jambo
Tumuogope na kumtii hakika kwake tutarejea



Ramadan Kareem

PATA FUNDISHO HAPAHapo zamani za kale, mwanamke mmoja mrembo aliyachoka maisha ya ndoa na alitaka kumuua mume wake. Siku...
20/02/2024

PATA FUNDISHO HAPA
Hapo zamani za kale, mwanamke mmoja mrembo aliyachoka maisha ya ndoa na alitaka kumuua mume wake.

Siku moja asubuhi alimkimbilia mama yake na kumwambia "mama nimemchoka mume wangu siwezi tena kuvumilia upuuzi wake nataka kumuua lakini naogopa Sheria ya nchi itanifunga, tafadhali unaweza kunisaidia?"

Mama yake akajibu:

- Ndio binti yangu naweza kukusaidia, lakini, kuna kazi ndogo utatakiwa kufanya.

Binti akauliza "kazi gani? Niko tayari na niko tayari kufanya kazi yoyote ili tu huyu mwanaume aondoke kwenye maishayangu"

Sawa, mama yake akakubali,

1..Itabidi urejeshe amani kwanza, ili mtu asije akakushuku siku akikutwa amekufa.

2.. Itabidi ujirembe ili uonekane binti na wa kuvutia kwake

3.. Unatakiwa kumtunza vizuri na kuwa mwenye shukrani kwake

4.. Unatakiwa kuwa mvumilivu, mwenye upendo na usiwe na wivu sana, uwe na masikio zaidi ya kusikiliza, kuwa na heshima na utii zaidi.

5. Tumia pesa yako kumuhudumia na usikasirike hata anapokosa pesa ya kununua chochote nyumbani..

6. Usipaze sauti yako dhidi yake bali penda Amani na upendo vitawale ili siku atakapokufa, watu wasikufikirie vibaya waone jinsi gani umempoteza mtu uliyekuwa unampenda...

" Je, unaweza kufanya yote hayo?". Mama yake aliuliza.

"Ndiyo naweza." Alijibu

"Sawa"

"Chukua unga huu na uwe unamwekea kila siku kwenye chakula chake, utakuwa unamuua polepole."

Baada ya siku 30 yule mwanamke alirudi kwa mama yake na kusema.

"Mama sina nia ya kumuua mume wangu tena. Kwa sasa ninampenda kwa sababu amebadilika kabisa, sasa ni mume mtamu sana kuliko nilivyofikiria.Je! nifanye nini kuzuia sumu isimuue? Tafadhali nisaidie mama." Aliomba kwa sauti ya huzuni.

Mama akajibu;

"Usijali binti yangu. Nilichokupa ni Unga wa kawaida tu. Hautamuua. Wewe ndiye ulikuwa sumu ambayo ilikuwa inamuua mumeo polepole kwa mikwaruzano na chuki uliyokuwa umeibeba. Ulipoanza kumpenda, kumuheshimu na kumthamini, ulimwokoa"

■Kuna kitu umepata hapa? | C&P

09/04/2023

Hii ndiyo sanaa ya ufikishaji. Hachoshi wala hachushi kumsikiliza.
Ninatamani aupige usenge kidogo.

29/03/2023
18/08/2022

*FUNGA YA JUMATATU NA AL'KHAMIS*

(( Ni siku ambazo Matendo ya Waja hupandishwa kwa Allah mtukufu }

_*Leo ni ((ALKHAMIS*))_
🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️

📃Imethibiti kwa Mtume (swallah allah aleyhi wassalam) alikuwa akifunga siku ya jumatatu na alkhamis, na sababu ya kuzichagua siku hizi mbili tu na isiwe siku nyingine k**a jumapili na na jumatano ni kuwa,
*siku hizi mbili ndio siku Ambazo matendo ya mja hunyanyuliwa au Hupelekwa kwa Allah mtukufu*..k**a ilivokuja katika hadithi aliyopokea abu hurayra..(radhwiya Allah anhu),

kwa Abu Hureira t kwamba Mtume ﷺ amesema:

( *تُعْرَضُ الأَعْمَالُ يَوْمَ الاثْنَيْنِ وَالْخَمِيسِ ؛ فَأُحِبُّ أَنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأَنَا صَائِمٌ] * رواه الترمذي]

*_Hupandishwa matendo (juu kwenda mbinguni) kila jumatatu na alhamisi, basi napenda matendo yangu yapandishwe hali ya kuwa nimefunga]_*
[Imepokewa na Tirmidhi.].

✍Pia Imekuja Katika hadithi nyingine aliyopokea qatadah (radhwiya Allah anhu) yenye nambari 1162 Katika Muslim, aliulizwa mtume kuhusiana swaumu ya siku ya jumatatu akasema "
_*"Ndio siku ambayo nimezaliwa pia ndio siku ambayo nimepewa utume"*

✍✍✍✍✍

*ELIMU KWA UMMA*

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255687080412

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ELIMU KWA UMMA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to ELIMU KWA UMMA:

Share